
kisha aliniachanisha na kugeuka ndipo aliponiona mimi akasema: "Laura? "Ndio mimi Laura " "Mbona upo hapa mpaka sasahivi si mmeruhusiwa kuondoka wewe imekuwaje umebaki hapa? "Nilikuwa nakungoja wewe General" "Mimi, kwanini? "Nilikuwa nataka kuongea na wewe General" "Haya niambie unataka kuongea kitu gani Laura? "Nikweli nakupenda sana General, japo nilikuwa nazikataa hisia zangu zakweli, lakini tangu umeondoka kambini hisia zangu juu yako zimezidi kuongezeka, nimeteseka sana sili silali nakumis sana mwenzio, kunamuda nilikuwa nalia tuu nikitamani kukuona ata kukusikia tuu japo sauti yako, moyo wangu umeondoka nao General nisamehe mimi nakuhitaji mno" Niliongea huku nikilia kwa hisia zandani ya moyo,
0 Comments