Anaamka saa 10 alfajiri, anakupa tendo la ndoa, wewe unarudi kulala, yeye anaingia moja kwa moja jikoni. Saa 11:30

asubuhi anaungana kwenye ibada ya asubuhi, saa 12:00 anaanza kuwaandaa watoto, saa 1:00 anawahudumia wote chakula, saa 1:30 anawapeleka watoto shule kisha anakwenda ofisini. Saa 8 mchana anarudi kuchukua watoto shuleni. Saa 11 jioni anarudi nyumbani, kuanzia saa 12 jioni anaanza kufua na kupika chakula cha jioni. Saa 1:30 usiku anahudumia chakula cha jioni, kisha kuanzia saa 2 hadi saa 3 usiku anashughulikia kazi za shule za watoto. Saa 3:30 usiku anaoga na kuungana na wewe mumewe chumbani, mnaongea na kufurahia ili kukuandaa uwe na hamu ya tendo la ndoa. Wewe mume, ukiwa na kichwa chako kikubwa, unalala kama mfalme.

Soma zaidi