
Tulitoka mbio na kuelekea pared, mara tuu baada ya kamanda kumaliza kuongea hivyo, tulikuwa kwenye mazoezi, vikosi vyote tulikutana hapo, na baada ya hapo tulifanya pared yanguvu kidogo, na kisha alisimama kiongozi wa vikosi vyote, tulimpa heshma kwa kutoa sarut, aliitikia nae kisha alisema: "Vikosi vyote makamanda, tunapaswa kufanya maandalizi, kwani kesho kutakuwa na ugeni, General Ethane atakuwa hapa, nadhani mnamjuwa, huwa hapendi makosa, hivyo tukitoka hapa wakuu wa vikosi wote tukutane ukumbi wa mkutano sawa"? Wakuu wa vikosi vyoote, waliitikia na kutii amli ya kiongozi, kisha tulipomaliza mazoezi ya pared, tuliruhusiwa tukaenda mabwenini, kwani muda wamazoezi pia ulikuwa umeisha,
0 Comments