
bwenini, niliumia kiasi kwamba nilishindwa hata kula chakula, nilipofika bwenini nilipanda kitandani na kulala, kiukweli Nancy pia alichukizwa na yale maongezi ya kina Catrine, ila alijizuia kuwafanyia timbwili aliwatizama tuu na kisha aliinuka na kuelekea bwenini nilipokuwa nimeenda mimi, alinikuta nimejilaza hapo kitandani akaniambia: "Laura tafadhari utafanya kilamtu ajue kuwa unampenda General, hembu fanya uzifiche hisia zako japo kidogo tuu" Nilikaa kimya sikumjibu kitu, ila Nancy aliendelea kusema: Naomba shuka chini twende ukale, haraka twende acha kuwa mjinga" Nikainuka na kumwambia Nancy huku machozi yakinitoka: "Unajua Nancy ninavyo mpenda General Ethane" "Najua kipenzi changu lakini usiwe hivyo, jikaze uitengeneze na
0 Comments