
na nilivyo mwembamba alafu Catrine alikuwa nanyama kidogo hivyo mkuu wakikosi alikuja haraka na kuninyanyua nisiendelee kumpiga Catrine nilikuwa naelewa basi nihasira tuu zimenipanda nilikuwa nasema: "Niache nimuonyeshe, atanizoea mimu huyu" Mkuu wakikosi alinishika kwa nguvu, huku akinizuia nisiende, na kuniambia: "Acha usiwe hivyo Laura , tulia nimesema tulia" Ndipo ikasikika sauti moja tuu sio kali ila alisema "Muachie tumuone" Nilishtuka, na kugeuka haraka kwani nisauti niliyokuwa naijua kabisa, kutizama vizuri alikuwa General, asikuambie mtu nilinywea kama kitunguu majii kwenye mafuta, General alisongea hadi nilipokuwa na kisha akasema: "Wewe tena" Nilibaki kimya siku mjibu kitu, nilisimama kwa nidhamu, nikiwa naogopa
0 Comments