
Sandra alihisi mikono ya Dkt. Mlenge ikishika yake kwa uthabiti lakini kwa upole wa ajabu. Hisia mchanganyiko zikazidi kumzonga hofu, aibu, na kitu fulani kisichoelezeka kilichokuwa kinamvuta karibu zaidi. Chumba kikabaki kimya, isipokuwa sauti ya kiyoyozi iliyokuwa ikivuma taratibu. Macho ya Dkt. Mlenge yalichoma ndani ya roho yake kana kwamba yalikuwa yanamvua nguo bila kumgusa. “Sandra…” alitamka taratibu, akimzungusha kidogo hadi uso wake utazame ule mlango wa chumba. “Kile nilichokuambia si utani. Ukikubali, unakuwa mmoja wetu… ukikataa, mlango uko pale.” Alibaki amenyamaza, akishusha pumzi ndefu. Akili yake ikipiga kelele: Niachane na hii, au nikubali na nipate ajira? Lakini mapigo ya
0 Comments