
wala hakujali Kuwa Mimi ni mwanamke wake lakini pia nimebeba Mtoto wake. Kipigo na maumivu vilinikolea mwisho nilipoteza fahamu kabisa. Baada ya hapo nilikuja kuamka baada ya masaa mawili baadae na nilijikuta nikiwa sebuleni, bado nilikuwa na maumivu makali sana na sehemu niliyokuwa nimelala kulikuwa na damu za kutosha na zilikuaa zikitokea kwenye sehemu zangu za Siri. “Mtoto wangu “ Nilizungumza kwa huzuni uku nikipapasa tumbo langu. Nikajikongoja na kutafuta simu yangu na nilipoipata tu nikampigia Rafiki yangu Yaani Yule Neha na kumuomba msaada ili aweze kunisaidia maana sikuwa na mtu mwingine na sikutaka kuwapa wasiwasi wazazi wangu ambao pia
0 Comments