𝗩𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗩𝗜𝗡𝗔𝗩𝗬𝗢𝗕𝗔𝗗𝗜𝗟𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗜𝗦𝗛𝗔 (𝗩𝗩𝗠) 𝗩𝗶𝗹𝗶𝘃𝘆𝗼𝗮𝗻𝗱𝗶𝗸𝘄𝗮 𝗡𝗮: 𝗔𝗦𝗞𝗢𝗙𝗨 𝗠𝗞𝗨𝗨 𝗭𝗔𝗖𝗛𝗔𝗥𝗬 𝗞𝗔𝗞𝗢𝗕𝗘
𝗩𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗩𝗜𝗡𝗔𝗩𝗬𝗢𝗕𝗔𝗗𝗜𝗟𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗜𝗦𝗛𝗔 (𝗩𝗩𝗠)
𝗩𝗶𝗹𝗶𝘃𝘆𝗼𝗮𝗻𝗱𝗶𝗸𝘄𝗮 𝗡𝗮:
𝗔𝗦𝗞𝗢𝗙𝗨 𝗠𝗞𝗨𝗨 𝗭𝗔𝗖𝗛𝗔𝗥𝗬 𝗞𝗔𝗞𝗢𝗕𝗘
Napenda kuchukua nafasi hii, kuwashukuru wanamaombi wote, kokote mlipo; ambao mmekuwa mkiiombea kazi hii ya Uandishi wa Vitabu; ambayo nimekuwa nikiifanya kwa muda sasa. Maombi yenu yameifanya kazi hii kubwa, kuendelea kwa ufanisi mkubwa, kwani kama wengi wetu tunavyofahamu; kazi hii isingewezekana kamwe kufanyika, pasipo maombi (YAKOBO 4:2; UFUNUO WA YOHANA 8:3-5). Zaidi sana, ninamshukuru Roho Mtakatifu, ambaye amekuwa akitufundisha njia itupasayo kuiendea, katika kuifanya kazi hii; na kutushauri, jicho lake likitutazama (ZABURI 32:8); na kuvifanya Vitabu hivi, kuandikwa kwa uvuvio wake; na uwezo wake wa kipekee (YOHANA 20:22; ZEKARIA 4:6; LUKA 24:49). Baada ya Shukurani hizi, nimeona vema pia, kuwapa ninyi wanamaombi mnaoiombea kazi hii; na pia kuwapa umma wote, kwa ujumla wake; mrejesho kuhusu maendeleo ya kazi hii ya Uandishi wa Vitabu, na hatua ilipofikia kwa sasa.
Kwanza kabisa, ni muhimu kuzingatia kwamba; Vitabu vilivyokamilika kuandikwa, na vingine vyote vinavyoendelea kuandikwa; siyo Vitabu vya hadithi zilizotungwa kwa werevu (2 PETRO 1:16), wala hadithi za maono na ndoto; zinazofananishwa na makapi au pumba, katika Maandiko; bali ni Vitabu vinavyolifafanua NENO LA MUNGU, na kulifanya liweze kueleweka kirahisi; na hivyo kulifanya Neno hilo kuweza kubadilisha maisha ya watu wengi, ambao hawawezi kulielewa Neno la Mungu bila kuongozwa, au kupewa ufafanuzi wa kina; kwa lugha nyepesi (MATENDO YA MITUME 8:27-34; YOHANA 15:3; YEREMIA 23:28-29). Ndiyo maana, Vitabu hivi vinaitwa "VITABU VINAVYOBADILISHA MAISHA". Ni Vitabu vya Neno la Mungu, lenye uwezo wa kubadilisha maisha ya wanadamu (WAEBRANIA 4:12-13).
Baada ya kuyajua haya, sasa ningependa kuwafahamisha wapendwa wangu; mahali ambapo kazi hii ya Uandishi wa Vitabu, ilipofikia. Hadi sasa, VITABU 16 VIMEKAMILIKA KUANDIKWA; na vimebakiza hatua chache tu za mwishoni, kabla ya uchapishaji wake. Orodha ifuatayo, ni ya Vitabu hivi 16, vilivyokamilika kuandikwa; ikiwa ni pamoja na Sura zake; na katika Sura mojawapo, nitavitaja Vipengele vyake; ili kukupa picha ya yale yaliyomo, japo kwa uchache.
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝐕𝐈𝐓𝐀𝐁𝐔 𝟏𝟔 𝐕𝐈𝐋𝐈𝐕𝐘𝐎𝐊𝐀𝐌𝐈𝐋𝐈𝐊𝐀 𝐊𝐔𝐀𝐍𝐃𝐈𝐊𝐖𝐀
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟭
𝐇𝐈𝐕𝐈 𝐊𝐖𝐄𝐋𝐈 𝐌𝐔𝐍𝐆𝐔 𝐘𝐔𝐏𝐎?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗛𝗜𝗩𝗜 𝗞𝗪𝗘𝗟𝗜
𝗠𝗨𝗡𝗚𝗨 𝗬𝗨𝗣𝗢?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗨𝗦𝗜𝗞𝗨 𝗛𝗨𝗨 𝗪𝗔 𝗟𝗘𝗢
𝗪𝗔𝗡𝗔𝗧𝗔𝗞𝗔
𝗥𝗢𝗛𝗢 𝗬𝗔𝗞𝗢!
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗞𝗜𝗟𝗔 𝗠𝗪𝗔𝗡𝗔𝗗𝗔𝗠𝗨
𝗔𝗠𝗘𝗪𝗘𝗞𝗘𝗪𝗔 𝗠𝗜𝗟𝗘𝗟𝗘
𝗡𝗗𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔𝗞𝗘
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟮
𝐘𝐀𝐍𝐀𝐘𝐎𝐉𝐈𝐑𝐈 𝐁𝐀𝐀𝐃𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐅𝐀
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗝𝗘! 𝗞𝗨𝗡𝗔 𝗠𝗔𝗜𝗦𝗛𝗔
𝗕𝗔𝗔𝗗𝗔 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗙𝗔?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗡𝗝𝗜𝗔 𝗡𝗬𝗘𝗠𝗕𝗔𝗠𝗕𝗔
𝗡𝗔 𝗡𝗝𝗜𝗔 𝗣𝗔𝗡𝗔
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗠𝗜𝗜𝗟𝗜 𝗬𝗔 𝗗𝗨𝗡𝗜𝗔𝗡𝗜 𝗡𝗔
𝗠𝗜𝗜𝗟𝗜 𝗬𝗔 𝗠𝗕𝗜𝗡𝗚𝗨𝗡𝗜
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟰 - 𝗦𝗔𝗙𝗔𝗥𝗜𝗡𝗜 𝗛𝗔𝗗𝗜
𝗣𝗔𝗥𝗔𝗗𝗜𝗦𝗢
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟱 - 𝗦𝗔𝗙𝗔𝗥𝗜𝗡𝗜 𝗛𝗔𝗗𝗜
𝗝𝗘𝗛𝗔𝗡𝗨𝗠 𝗬𝗔 𝗠𝗢𝗧𝗢
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟲 - 𝗪𝗘𝗡𝗚𝗜 𝗪𝗔𝗧𝗔𝗧𝗔𝗞𝗔
𝗞𝗨𝗜𝗡𝗚𝗜𝗔 𝗠𝗕𝗜𝗡𝗚𝗨𝗡𝗜
𝗟𝗔𝗞𝗜𝗡𝗜 𝗪𝗔𝗦𝗜𝗪𝗘𝗭𝗘
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟳 - 𝗠𝗧𝗨 𝗔𝗙𝗔𝗡𝗬𝗘𝗝𝗘
𝗕𝗔𝗦𝗜 𝗜𝗟𝗜 𝗔𝗪𝗘𝗭𝗘
𝗞𝗨𝗜𝗡𝗚𝗜𝗔 𝗠𝗕𝗜𝗡𝗚𝗨𝗡𝗜?
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟯
𝐔𝐙𝐔𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐁𝐈𝐍𝐆𝐔𝐍𝐈
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗨𝗙𝗨𝗡𝗨𝗢 𝗞𝗨𝗛𝗨𝗦𝗨
𝗨𝗭𝗨𝗥𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗕𝗜𝗡𝗚𝗨𝗡𝗜
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗝𝗘, 𝗠𝗕𝗜𝗡𝗚𝗨𝗡𝗜
𝗡𝗜 𝗪𝗔𝗣𝗜?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗝𝗜𝗡𝗦𝗜 𝗠𝗕𝗜𝗡𝗚𝗨𝗡𝗜
𝗞𝗨𝗟𝗜𝗩𝗬𝗢 𝗞𝗨𝗭𝗨𝗥𝗜
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟰 - 𝗝𝗜𝗡𝗦𝗜 𝗠𝗔𝗜𝗦𝗛𝗔
𝗬𝗔𝗟𝗜𝗩𝗬𝗢 𝗠𝗕𝗜𝗡𝗚𝗨𝗡𝗜
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟱 - 𝗝𝗜𝗡𝗦𝗜 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗜𝗡𝗚𝗜𝗔
𝗠𝗕𝗜𝗡𝗚𝗨𝗡𝗜
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟰
𝐅𝐀𝐒𝐈𝐑𝐈 𝐒𝐀𝐇𝐈𝐇𝐈 𝐘𝐀 𝐍𝐄𝐍𝐎 "𝐔𝐒𝐈𝐇𝐔𝐊𝐔𝐌𝐔"
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗪𝗔𝗝𝗜𝗕𝗨 𝗪𝗔 𝗞𝗨𝗟𝗜𝗙𝗔𝗦𝗜𝗥𝗜
𝗡𝗘𝗡𝗢 𝗟𝗔 𝗠𝗨𝗡𝗚𝗨
𝗞𝗪𝗔 𝗨𝗦𝗔𝗛𝗜𝗛𝗜
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗙𝗔𝗦𝗜𝗥𝗜 𝗜𝗦𝗜𝗬𝗢 𝗦𝗔𝗛𝗜𝗛𝗜
𝗬𝗔 𝗡𝗘𝗡𝗢 "𝗨𝗦𝗜𝗛𝗨𝗞𝗨𝗠𝗨"
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗙𝗔𝗦𝗜𝗥𝗜 𝗦𝗔𝗛𝗜𝗛𝗜
𝗬𝗔 𝗡𝗘𝗡𝗢 "𝗨𝗦𝗜𝗛𝗨𝗞𝗨𝗠𝗨"
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟱
𝐌𝐓𝐄𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐃𝐈𝐍𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐃𝐇𝐄𝐇𝐄𝐁𝐔
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗬𝗘𝗦𝗨 𝗞𝗥𝗜𝗦𝗧𝗢
𝗛𝗔𝗞𝗨𝗟𝗘𝗧𝗔 𝗗𝗜𝗡𝗜
𝗔𝗨 𝗗𝗛𝗘𝗛𝗘𝗕𝗨 𝗟𝗢𝗟𝗢𝗧𝗘
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗗𝗜𝗡𝗜 𝗡𝗔 𝗠𝗔𝗗𝗛𝗘𝗛𝗘𝗕𝗨
𝗔𝗗𝗨𝗜 𝗪𝗔𝗞𝗨𝗨 𝗪𝗔 𝗬𝗘𝗦𝗨 𝗞𝗥𝗜𝗦𝗧𝗢
𝗡𝗔 𝗪𝗔𝗡𝗔𝗙𝗨𝗡𝗭𝗜 𝗪𝗔𝗞𝗘
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗠𝗧𝗘𝗚𝗢 𝗪𝗔 𝗗𝗜𝗡𝗜 𝗡𝗔
𝗠𝗔𝗗𝗛𝗘𝗛𝗘𝗕𝗨 𝗡𝗔
𝗝𝗜𝗡𝗦𝗜 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗨𝗞𝗪𝗘𝗣𝗔
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟲
𝐔𝐊𝐑𝐈𝐒𝐓𝐎 𝐈𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐓𝐔 𝐏𝐄𝐊𝐄 𝐘𝐀𝐊𝐄
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗞𝗨𝗔𝗡𝗗𝗜𝗞𝗪𝗔 𝗞𝗔𝗧𝗜𝗞𝗔
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗖𝗛𝗔 𝗨𝗭𝗜𝗠𝗔
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗨𝗞𝗥𝗜𝗦𝗧𝗢 𝗜𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔
𝗠𝗧𝗨 𝗣𝗘𝗞𝗘 𝗬𝗔𝗞𝗘
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗦𝗔𝗙𝗔𝗥𝗜 𝗬𝗔 𝗣𝗘𝗞𝗘 𝗬𝗔𝗞𝗢
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟰 - 𝗞𝗨𝗪𝗔 𝗡𝗔 𝗠𝗦𝗜𝗠𝗔𝗠𝗢
𝗪𝗔 𝗣𝗘𝗞𝗘 𝗬𝗔𝗞𝗢
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟳
𝐉𝐈𝐍𝐒𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐇𝐈𝐍𝐃𝐀 𝐃𝐇𝐀𝐌𝐁𝐈
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗗𝗛𝗔𝗠𝗕𝗜 𝗡𝗜 𝗡𝗜𝗡𝗜?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗨𝗕𝗔𝗬𝗔 𝗪𝗔 𝗗𝗛𝗔𝗠𝗕𝗜
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗞𝗨𝗪𝗘𝗭𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗞𝗨𝗪𝗘𝗭𝗘𝗦𝗛𝗪𝗔
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟴
𝐌𝐓𝐔 𝐀𝐒𝐈𝐏𝐎𝐙𝐀𝐋𝐈𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐏𝐈𝐋𝐈
𝐇𝐀𝐖𝐄𝐙𝐈 𝐊𝐔𝐈𝐍𝐆𝐈𝐀 𝐌𝐁𝐈𝐍𝐆𝐔𝐍𝐈
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗡𝗜𝗡𝗜 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗔 𝗬𝗔
𝗞𝗨𝗭𝗔𝗟𝗜𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗥𝗔 𝗬𝗔 𝗣𝗜𝗟𝗜?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗦𝗜𝗙𝗔 𝗕𝗔𝗜𝗡𝗜𝗙𝗨 𝗭𝗔 𝗠𝗧𝗨
𝗔𝗠𝗕𝗔𝗬𝗘 𝗛𝗔𝗝𝗔𝗭𝗔𝗟𝗜𝗪𝗔
𝗠𝗔𝗥𝗔 𝗬𝗔 𝗣𝗜𝗟𝗜
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗝𝗜𝗡𝗦𝗜 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗭𝗔𝗟𝗜𝗪𝗔
𝗠𝗔𝗥𝗔 𝗬𝗔 𝗣𝗜𝗟𝗜
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟵
𝐍𝐈𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐎𝐊𝐎𝐊𝐀?
● 𝐉𝐞! 𝐊𝐰𝐞𝐥𝐢 𝐖𝐞𝐰𝐞 𝐔𝐦𝐞𝐨𝐤𝐨𝐤𝐚?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗡𝗜𝗡𝗜 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗔 𝗬𝗔
𝗞𝗨𝗢𝗞𝗢𝗞𝗔?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗝𝗘, 𝗞𝗨𝗢𝗞𝗢𝗞𝗔
𝗡𝗜 𝗛𝗔𝗣𝗔𝗛𝗔𝗣𝗔
𝗗𝗨𝗡𝗜𝗔𝗡𝗜?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗞𝗨𝗢𝗡𝗚𝗢𝗞𝗔
𝗡𝗔 𝗞𝗨𝗢𝗞𝗢𝗞𝗔
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟰 - 𝗞𝗨𝗢𝗞𝗢𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔
𝗡𝗝𝗜𝗔 𝗬𝗔 𝗜𝗠𝗔𝗡𝗜
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠- 𝟭𝟬
𝐓𝐎𝐅𝐀𝐔𝐓𝐈 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐒𝐇𝐈𝐊𝐀 𝐃𝐈𝐍𝐈 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐎𝐊𝐎𝐊𝐀
● 𝐌𝐟𝐚𝐧𝐨 𝐰𝐚 𝐁𝐚𝐝𝐢𝐥𝐢𝐤𝐨 𝐥𝐚 𝐒𝐚𝐮𝐥𝐢
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗕𝗔𝗗𝗜𝗟𝗜𝗞𝗢 𝗟𝗔 𝗦𝗔𝗨𝗟𝗜
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗝𝗜𝗡𝗦𝗜 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗣𝗔𝗧𝗔
𝗕𝗔𝗗𝗜𝗟𝗜𝗞𝗢 𝗟𝗔 𝗦𝗔𝗨𝗟𝗜
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟭𝟭
𝐈𝐒𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐌𝐁𝐈𝐋𝐈 𝐙𝐀 𝐌𝐒𝐈𝐍𝐆𝐈 𝐙𝐀 𝐊𝐔𝐙𝐀𝐋𝐈𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐏𝐈𝐋𝐈
● 𝐊𝐮𝐲𝐚𝐜𝐡𝐮𝐤𝐢𝐚 𝐔𝐥𝐢𝐲𝐨𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐔𝐧𝐚𝐲𝐚𝐩𝐞𝐧𝐝𝐚
● 𝐊𝐮𝐲𝐚𝐩𝐞𝐧𝐝𝐚 𝐔𝐥𝐢𝐲𝐨𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐔𝐧𝐚𝐲𝐚𝐜𝐡𝐮𝐤𝐢𝐚
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗜𝗦𝗛𝗔𝗥𝗔 𝗠𝗕𝗜𝗟𝗜 𝗭𝗔 𝗠𝗦𝗜𝗡𝗚𝗜 𝗭𝗔
𝗞𝗨𝗭𝗔𝗟𝗜𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗥𝗔 𝗬𝗔 𝗣𝗜𝗟𝗜
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗠𝗨𝗨𝗝𝗜𝗭𝗔 𝗪𝗔 𝗞𝗨𝗭𝗔𝗟𝗜𝗪𝗔
𝗠𝗔𝗥𝗔 𝗬𝗔 𝗣𝗜𝗟𝗜
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟭𝟮
𝐉𝐄! 𝐓𝐔𝐅𝐀𝐍𝐘𝐄 𝐃𝐇𝐀𝐌𝐁𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐒𝐀𝐁𝐀𝐁𝐔 𝐓𝐔𝐊𝐎
𝐂𝐇𝐈𝐍𝐈 𝐘𝐀 𝐍𝐄𝐄𝐌𝐀?
● 𝐍𝐢𝐧𝐢 𝐦𝐚𝐚𝐧𝐚 𝐲𝐚 𝐍𝐞𝐞𝐦𝐚?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗝𝗘! 𝗧𝗨𝗙𝗔𝗡𝗬𝗘 𝗗𝗛𝗔𝗠𝗕𝗜
𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗔𝗕𝗔𝗕𝗨
𝗧𝗨𝗞𝗢 𝗖𝗛𝗜𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗡𝗘𝗘𝗠𝗔?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗧𝗢𝗥𝗔𝗧𝗜 𝗬𝗔 𝗠𝗨𝗦𝗔 𝗔𝗨
𝗦𝗛𝗘𝗥𝗜𝗔 𝗬𝗔 𝗠𝗨𝗦𝗔
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗡𝗘𝗘𝗠𝗔 𝗡𝗔 𝗞𝗪𝗘𝗟𝗜
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟰 - 𝗡𝗘𝗘𝗠𝗔 𝗝𝗨𝗨 𝗬𝗔 𝗡𝗘𝗘𝗠𝗔
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟭𝟯
𝐍𝐈𝐍𝐈 𝐌𝐀𝐀𝐍𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐌𝐊𝐈𝐑𝐈 𝐘𝐄𝐒𝐔 𝐊𝐑𝐈𝐒𝐓𝐎 𝐘𝐀
𝐊𝐔𝐖𝐀 𝐍𝐈 𝐁𝐖𝐀𝐍𝐀?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗕𝗪𝗔𝗡𝗔 𝗡𝗔 𝗠𝗪𝗢𝗞𝗢𝗭𝗜
𝗬𝗘𝗦𝗨 𝗞𝗥𝗜𝗦𝗧𝗢
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗡𝗜𝗡𝗜 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗔 𝗬𝗔
𝗞𝗨𝗠𝗞𝗜𝗥𝗜 𝗬𝗘𝗦𝗨 𝗞𝗥𝗜𝗦𝗧𝗢
𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗪𝗔 𝗡𝗜 𝗕𝗪𝗔𝗡𝗔?
● 1. Kumkiri Yesu Kristo, ya kuwa ni BWANA; ni kumkubali Yesu kuwa ni Kamanda Mkuu au Amirijeshi Mkuu wa Majeshi yake yote, yaliyoko mbinguni na duniani; na wewe ni Askari wake.
● 2. Kumkiri Yesu Kristo, ya kuwa, ni BWANA; ni kumkubali Yesu ya kuwa ni BWANA, na wewe ni Mtumwa wake, usiye na faida.
● 3. Kumkiri Yesu Kristo, ya kuwa, ni BWANA; ni kumkubali Yesu, ya kuwa ni MMILIKI wako, na wewe, pamoja na vyote ulivyo, ni mali yake.
● 4. Kumkiri Yesu Kristo, ya kuwa ni BWANA; ni kumkubali Yesu, ya kuwa ni MFALME WA WAFALME, na Bwana wako Mfalme; na pia Mfalme wako wa milele; na wewe ni mtu wake, anayekutawala.
● 5. Kumkiri Yesu Kristo, ya kuwa ni BWANA; ni kumkubali Yesu, ya kuwa, Ndiye Mwamuzi au Jaji wako atakayekuhukumu; na pia Ndiye Mfanya sheria au Mtoa sheria wako, na wajibu wako wewe ni kuzitekeleza sheria zake.
● 6. Kumkiri Yesu Kristo, ya kuwa ni BWANA; ni kumkubali Yesu, ya kuwa, Ndiye Nahodha au Kiongozi Mkuu wa safari yako ya wokovu; na ni wajibu wako wewe, kukubali kuongozwa na Yesu, na kuyategemea maongozi Yake, katika safari yako ya kwenda mbinguni.
●7. Kumkiri Yesu Kristo, ya kuwa ni BWANA; ni kumkubali Yesu, ya kuwa, Yeye Ndiye MWALIMU WAKO MMOJA TU unayepaswa kujifunza kwake, na kumfuata, katika maisha yako yote ya wokovu ; ukizingatia kwamba wewe ni Mwanafunzi wake; na kwamba, waalimu wengine wote, unajifunza kwao na kuwafuata; kama na wao pia, wanavyojifunza kwake Kristo, na kumfuata.
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟭𝟰
𝐇𝐈𝐕𝐈 𝐊𝐖𝐄𝐋𝐈 𝐖𝐄𝐖𝐄 𝐔𝐍𝐀𝐌𝐏𝐄𝐍𝐃𝐀 𝐘𝐄𝐒𝐔?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗔 𝗛𝗔𝗟𝗜𝗦𝗜 𝗬𝗔
𝗞𝗨𝗠𝗣𝗘𝗡𝗗𝗔 𝗬𝗘𝗦𝗨
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗝𝗘! 𝗪𝗔𝗡𝗜𝗣𝗘𝗡𝗗𝗔,
𝗞𝗨𝗟𝗜𝗞𝗢 𝗛𝗔𝗪𝗔?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗞𝗔𝗠𝗔 𝗡𝗜 𝗛𝗜𝗩𝗬𝗢
𝗡𝗔 𝗞𝗔𝗠𝗔 𝗦𝗜 𝗛𝗜𝗩𝗬𝗢
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟰 - 𝗝𝗜𝗡𝗦𝗜 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗠𝗣𝗘𝗡𝗗𝗔
𝗬𝗘𝗦𝗨 𝗞𝗪𝗔 𝗗𝗛𝗔𝗧𝗜
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟭𝟱
𝐊𝐖𝐀 𝐍𝐈𝐍𝐈 𝐔𝐁𝐀𝐓𝐈𝐙𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐉𝐈 𝐓𝐄𝐋𝐄?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗡𝗜𝗡𝗜 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗔 𝗬𝗔
𝗡𝗘𝗡𝗢 𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗝𝗘! 𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗜
𝗨𝗡𝗔𝗢𝗡𝗗𝗢𝗔 𝗗𝗛𝗔𝗠𝗕𝗜 𝗡𝗔
𝗞𝗨𝗠𝗙𝗔𝗡𝗬𝗔 𝗠𝗧𝗨 𝗔𝗭𝗔𝗟𝗜𝗪𝗘
𝗠𝗔𝗥𝗔 𝗬𝗔 𝗣𝗜𝗟𝗜 𝗡𝗔 𝗞𝗨𝗢𝗞𝗢𝗞𝗔?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟯 - 𝗝𝗘, 𝗪𝗔𝗧𝗢𝗧𝗢 𝗪𝗔𝗗𝗢𝗚𝗢
𝗡𝗔𝗢 𝗪𝗔𝗡𝗔𝗧𝗔𝗞𝗜𝗪𝗔
𝗞𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗪𝗔
𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗜?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟰 - 𝗝𝗘, 𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢 𝗪𝗔
𝗥𝗢𝗛𝗢 𝗠𝗧𝗔𝗞𝗔𝗧𝗜𝗙𝗨
𝗨𝗡𝗔𝗢𝗡𝗗𝗢𝗔 𝗨𝗠𝗨𝗛𝗜𝗠𝗨
𝗪𝗔 𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗜?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟱 - 𝗠𝗧𝗜𝗛𝗔𝗡𝗜 𝗪𝗔 𝗞𝗪𝗔𝗡𝗭𝗔
𝗪𝗔 𝗨𝗧𝗜𝗜 𝗞𝗪𝗔 𝗪𝗔𝗧𝗢𝗧𝗢
𝗪𝗔 𝗞𝗨𝗧𝗜𝗜
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟲 - 𝗧𝗘𝗡𝗗𝗢 𝗟𝗜𝗡𝗔𝗟𝗢𝗔𝗞𝗜𝗦𝗜
𝗜𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗙𝗔
𝗞𝗨𝗭𝗜𝗞𝗪𝗔 𝗡𝗔 𝗞𝗨𝗙𝗨𝗙𝗨𝗞𝗔
𝗞𝗪𝗔 𝗬𝗘𝗦𝗨 𝗞𝗥𝗜𝗦𝗧𝗢
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟳 - 𝗝𝗘, 𝗪𝗔𝗧𝗨 𝗛𝗔𝗪𝗔
𝗪𝗔𝗟𝗜𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗪𝗔 𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢
𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗜 𝗧𝗘𝗟𝗘?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟴 - 𝗠𝗕𝗢𝗡𝗔 𝗠𝗛𝗔𝗟𝗜𝗙𝗨 𝗠𝗦𝗔𝗟𝗔𝗕𝗔𝗡𝗜
𝗛𝗔𝗞𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗪𝗔 𝗟𝗔𝗞𝗜𝗡𝗜
𝗔𝗟𝗜𝗘𝗡𝗗𝗔 𝗠𝗕𝗜𝗡𝗚𝗨𝗡𝗜?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟵 - 𝗝𝗘, 𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗜
𝗨𝗡𝗔𝗙𝗔𝗡𝗬𝗜𝗞𝗔 𝗞𝗪𝗔
𝗝𝗜𝗡𝗔 𝗚𝗔𝗡𝗜?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭𝟬 - 𝗝𝗘, 𝗠𝗧𝗨 𝗔𝗡𝗔𝗣𝗢𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗪𝗔
𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗜 𝗡𝗜 𝗟𝗔𝗭𝗜𝗠𝗔
𝗔𝗕𝗔𝗗𝗜𝗟𝗜𝗦𝗛𝗘 𝗝𝗜𝗡𝗔?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭𝟭 - 𝗡𝗜 𝗡𝗔𝗡𝗜 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗬𝗘 𝗦𝗜𝗙𝗔
𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗔 𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗢
𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗜?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭𝟮 - 𝗠𝗔𝗦𝗪𝗔𝗟𝗜 𝗠𝗘𝗡𝗚𝗜𝗡𝗘
𝗬𝗔𝗡𝗔𝗬𝗢𝗨𝗟𝗜𝗭𝗪𝗔
𝗠𝗔𝗥𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗥𝗔
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭𝟯 - 𝗝𝗘, 𝗡𝗜 𝗦𝗔𝗛𝗜𝗛𝗜 𝗞𝗨𝗕𝗔𝗧𝗜𝗭𝗪𝗔
𝗭𝗔𝗜𝗗𝗜 𝗬𝗔 𝗠𝗔𝗥𝗔 𝗠𝗢𝗝𝗔?
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭𝟰 - 𝗪𝗔𝗝𝗜𝗕𝗨 𝗪𝗔 𝗞𝗨𝗙𝗔𝗡𝗬𝗔
𝗛𝗔𝗥𝗔𝗞𝗔 𝗞𝗨𝗧𝗜𝗜
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
𝗞𝗜𝗧𝗔𝗕𝗨 𝗡𝗔𝗠𝗕𝗔: 𝗩𝗩𝗠-𝟭𝟲
𝐌𝐔𝐔𝐉𝐈𝐙𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐁𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐈𝐊𝐎 𝐌𝐈𝐔𝐉𝐈𝐙𝐀 𝐘𝐎𝐓𝐄: 𝐌𝐔𝐔𝐉𝐈𝐙𝐀 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐔𝐌𝐁𝐖𝐀 𝐔𝐏𝐘𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐔𝐌𝐁𝐄 𝐊𝐈𝐏𝐘𝐀
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟭 - 𝗠𝗜𝗨𝗝𝗜𝗭𝗔 𝗔𝗠𝗕𝗔𝗬𝗢 𝗡𝗜
𝗖𝗛𝗔𝗞𝗨𝗟𝗔 𝗖𝗛𝗘𝗡𝗬𝗘 𝗞𝗨𝗛𝗔𝗥𝗜𝗕𝗜𝗞𝗔
𝗦𝘂𝗿𝗮 𝘆𝗮 𝟮 - 𝗠𝗨𝗨𝗝𝗜𝗭𝗔 𝗠𝗞𝗨𝗕𝗪𝗔 𝗞𝗨𝗟𝗜𝗞𝗢 𝗠𝗜𝗨𝗝𝗜𝗭𝗔 𝗬𝗢𝗧𝗘:
𝗠𝗨𝗨𝗝𝗜𝗭𝗔 𝗪𝗔 𝗞𝗨𝗨𝗠𝗕𝗪𝗔 𝗨𝗣𝗬𝗔
𝗡𝗔 𝗞𝗨𝗪𝗔 𝗞𝗜𝗨𝗠𝗕𝗘 𝗞𝗜𝗣𝗬𝗔
■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■■
Bila shaka, Vitabu hivi 16 vilivyokamilika kuandikwa; pamoja na makumi ya Vitabu vingine vinavyoendelea kuandikwa; ambavyo viko katika hatua mbalimbali tofauti; vitakuwa msaada mkubwa kwa mamilioni ya watu wanaofahamu lugha ya Kiswahili, katika kuwaandaa kujiweka tayari kuonana na Mungu (AMOSI 4:12); na pia katika kulisafisha Kanisa la Mungu, kwa maji katika Neno, na kuliandaa kwa tukio ambalo liko karibu sana, la Kunyakuliwa kwa Kanisa; au Kunyakuliwa kwa Watakatifu (WAEFESO 5:25-27; 1 WATHESALONIKE 4:15-17; LUKA 17:26-30, 34-36; MATHAYO 24:37-44; WAEBRANIA 10:37; UFUNUO WA YOHANA 22:12).
Aidha, ni muhimu kuzingatia kwamba; ingawa Vitabu hivi 16 vimekamilika kuandikwa, na vimebakiza hatua chache za mwisho mwisho, kabla ya uchapishaji wake; hata hivyo Vitabu hivi, havitaingizwa sokoni kwanza, mpaka SETI YA KWANZA ya Vitabu hivi, itakapotimia; itakayokuwa na Vitabu mbalimbali vya msingi, vitakavyomwezesha Msomaji aliyeanza safari ya wokovu; kuukulia wokovu wake, na kuwa siyo tu nuru ya ulimwengu (MATHAYO 5:14-16); bali pia kuwa Mwanafunzi wa Yesu aliyeimarika vema kiroho, asiyeweza kutikiswa kirahisi na roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; ya nyakati hizi za mwisho (1 WAKORINTHO 15:58; 1 TIMOTHEO 4:1). Kazi hii ya Uandishi wa Vitabu, bado inaendelea kwa bidii yote, ili kutimiza Vitabu vya Seti ya Kwanza; na ninachoomba tu kwako, ni kuzidi kuuchochea moto wa kazi hii kwa kuni, ambazo ni maombi (MITHALI 26:20; 1 WATHESALONIKE 5:25). Baada ya taarifa hii, ninajua baadhi yenu tayari, mna shauku kubwa ya kuvipata Vitabu hivi; hata hivyo, twawaita heri, yaani wamebarikiwa watu walio na subira (YAKOBO 5:11).
Nazidi kusema Asante sana kwa ushirikiano wako. Tukidumu katika umoja wetu; na tukizidi kumshirikisha Mungu wetu katika kazi hii, kwa maombi; kwa hakika twaweza kutenda mambo makuu! (DANIELI 11:32).
Pamoja sana!
Ni mimi mjoli wenu na mtumishi wenu,
𝑨𝒔𝒌𝒐𝒇𝒖 𝑴𝒌𝒖𝒖 𝒁𝒂𝒄𝒉𝒂𝒓𝒚 𝑲𝒂𝒌𝒐𝒃𝒆

Comments
Post a Comment