
PENZI LA SINGLE MAMA SEHEMU YA 5 Tunaendelea pale pale tulipoishia baada ya Maria kujiuliza sana maswali kuhusu mwanaume anayemsaidia mtoto wake ambaye kichwani mwa mwanaye anafahamika kama mjomba . Alijiuliza sana Maria kuhusu huyo mwanaume mwenye huruma,mwenye kujali mtoto wake na mwenye kumjali yeye ingawa hata hamfahamu. Alijisemea " MUNGU akuzishie baraka na akupe maisha marefu ,maana katika dunia hii ni ngumu mtu kumjali mtu asiyemfahamu. Natumai siku moja nitakuona kaka" Basi asijuwe kuwa mimi ndo ninayemsaidia mwanaye na hata dawa vyote nimefanya mimi. Huku hata akili yangu inawaza nitaona na maria lini na nilijiuliza kwa nini
0 Comments