
"Nyama ni nyama tu kikubwa iwe imeiva acha kutengeneza taharuki masikioni mwangu" Levi aliongea huku akizidisha kutembea. "Tembea taratibu sasa lakini utake usitake Amelia ndio ameshakuwa mke wako. Nitahakikisha hamuachani yaani Mimi hapa nitawapambania kama watoto yatima vile wanaodai haki zao" Henry aliongea. Levi alizidi kusikia hasira kuna namna alitamani kumpiga Henry lakini kwa kuwa ni Mjomba wake alivumilia. "Amelia ni binti mrembo sana nipo radhi nipoteze macho yangu kutetea penzi lenu...." Henry alizidi kuongea, alipoona Levi hamjali aliamua kupaza sauti kabisa. "Watuuuu, Levi ni Mume wa Amelia msikubali atembee na Dada zenu au watoto zenu... Mume wa mtu ni
0 Comments