
SEHEMU YA 1 "Ni kusema umechoka kazi Tunu?...hapa ni Uturuki na si Tanzania! kadri unavyozidi kufanya kazi vibaya ndivyo unavyo jichelewesha mshahara wako.....usiniambie mpaka sasa hujui matumizi ya sukari kwanini uweke sukari kwenye supu badala ya chumvi" Bi. Rahma alifoka Sikutaka kuamini maneno yake, hata kama nina ushamba kiasi gani siwezi kusahau matumizi ya sukari. Nilichukua kijiko ni kaonjo supu kidogo. Halooo sukari ilizidi kuliko chumvi niliyokuwa nimeweka "Naomba unisamehe lakini nina akili timamu siwezi kuweka sukari kwenye supu" Nilijitetea "Kwahiyo Mimi ndio nimeweka sukari kwenye supu si ndiyo" Bi. Rahma aliuliza akiwa kakunja uso wake "Sijamaanisha hivyo..." "Ooh unataka
0 Comments