
kisha akampigia simu secretary wake. “Chukua kijana huyu mpeleke kwenye chumba cha michezo, ajiburudishe.” Adam alitabasamu na kumwangalia mama yake. “Usijali, mama. Nitakagua kama huyu boss ni baba mzuri kweli,” akasema huku akitoka kwa utundu. Mara tu mlango ulipofungwa, Damian aligeuza macho yake makali kwa Amina. Ofisi nzima ilijaa ukimya mzito, na pumzi ya Amina ikawa nzito zaidi. “Kwa hiyo, Bi. Amina,” Damian alianza kwa sauti ya taratibu lakini yenye mamlaka, “umerejea Tanzania baada ya miaka minane. Na sasa unataka kazi katika kampuni yangu?” Amina akajikaza, akiinua macho yake. “Ndio, Bwana Damian. Niko tayari kufanya kazi kwa bidii. Hii nafasi
0 Comments