
Angejua mwenzie nilikimbia shule wala asingejihangaisha kuniandikia vingereza🥺.. Alichokiandika sikukielewa hata kidogo😂😂😂nilijikuna kuna kichwa pale mmhh kumwambia sielewi naona aibu nyiee🤣🤣 Kingston muda wote akawa ananiangalia alafu cha ajabu akawa hafanyi zile tabia za kizezeta alikuwa amesimama kiustaarabu kama mtu asiyeumwa chochote😳😳😳.. Nilistaajabu baada ya kumuona alivyosimama kwa kutulia but ni kama alijisahau tu maana aliponiona namshangaa alianza kujitililishia udenda na kuiweka ile mikono yake kama chizi kawaona ndugu zake🥺🥺🥺.. Mmhh kuna kasintofahamu nikaanza kuwa nako juu ya Boy mbona kama huu ugonjwa wake ni wa maigizo😳😳😳 Kwanza jana usiku wakati tunaomba nilipofungua macho naye alikuwa anatuangalia akiwa timamu kabisa🥺🥺🥺
0 Comments