
Sisi tupo salama ila baba yako alipigwa na mabapa ya panga. Walimlazimisha baba yako akafungua shelfu wakachukua document za muhumu sijui itakuwaje kila kitu chetu kipo mule. Ni mwana haramu gani kafanya haya? Wamechukua nini? Huu ni mpango kuna mtu yupo nyuma ya hili. Baada ya kuongea na mama yake alienda kumchukua salsa kwenye gari na kumpeleka kwa mama yake. *Shikamoo mama. *Marahaba. *Mama huyu ndio mkwe wako nae kwa upande wake mambo hayapo sawa ndio maana nimekuja nae hapa. Karibu nyumbani mwanangu. * Usijali mwanangu, umefanya jambo la maana. *Asante mama, poleni kwa matatizo. Asante. Wakiwa bado wanaongea walipata
0 Comments