
Simulizi za john 0789 824 178 , 1000 Nikasema, “Mama, hakuna chochote, baba alikuwa anaangalia vidonda tu.” Akasema, “Unasemaje? Baba? Baba gani? Babako yule? Unamudu ili unibadilishe uishi kwenye ghorofa hii, si ndiyo? Unaona ninafaidi, unataka kuwa mke mwenza, si ndiyo? Ulimuonyesha nini huko chini?” Nikasema, “Mama, mbona unaniambia maneno ambayo sielewi? Unanionea!” Akasema, “Nani anakunea?” Alinishika, akanibamiza ukutani, akasema, “Nitakuua!” Nilipasuka kichwani kisogoni, damu zikamwagika. Mama hakustuka, akaendelea kunipiga, kisha akasema, “Toka kwangu, toka!” Akanisukuma nje huku navuja damu, nalia, bila kusema nisamehe—nilishaamua kuondoka, bora nikafie mbali. Nikimkumbuka mama na bibi yangu, nilitamani kurudi, lakini baba yangu ni mkatili,
0 Comments