
Kwa presha ambayo Mama huyo alikuwa nayo pale pale alizimia, hakika Mr Tamir alihisi Dunia inazunguka, yaani jasho kwenye ukwapa lilimjaa haswa. Kwanza ilibidi Aite wafanyakazi wake wasaidiane kumukimbiza Mkewe hospital. Mr Tamir alikuwa kachanganyikiwa kuliko kawaida. Masaa hayo hayo alianza kufanya mchakato Wa kuwasiliana na wahusika walio ifunga akaunti ya Jovin, maana Yeye ndo alikuwa katoa vihongo mpaka ikawa vile!. Japo kulikuwa na ugumu Wake kueleweka, ila kwa Sababu alikuwa anatumia Pesa Hiyo aliambiwa asubiri Baada ya Masaa 24 akaunti itakuwa ipo Sawa!. Kurudisha nyaraka ilikuwa Siyo Kazi kwa Sababu Mr Tamir alikuwa nazo nyumbani kwake na kizuri na
0 Comments