
ametanguliza makalio huyu! Inabidi tufanye hima isipite leo auwawe na nyama zake tuzile, yani tufanye kila mbinu hata kwa kutumia uchawi wa ukoo wetu" waze waliobaki msibani walijadilana baada ya Bryton na Rabia kuondoka msibani wakirejea mjini. Walipofika tu mjini, Rabia alipigiwa simu na kualikwa kwenye semina ya wafanya biashara matajiri jiji Arusha. "Kaka Bryton nimealikwa kwenye semina ya wafanyabiasha ambayo inafanyika jioni twende wote au unasemaje kaka" Rabia alimuuliza Bryton. "Sawa hakuna shida dada tunaweza tu kuondoka" Alisema Bryton. Basi jioni ile wakapitia RABIA HOTEL VIEW PACK wakapata msosi kisha Rabia akamtambulisha Bryton kwa wafanyakazi wake. "Jamani huyu ni
0 Comments