π‰π€πŒπ€ππˆ ππŽπ’π’ 𝐌𝐈 ππ€πŽππ€ π€πˆππ” πŸ’πŸ™ˆπŸ’ž: 76

π‰π€πŒπ€ππˆ ππŽπ’π’ 𝐌𝐈 ππ€πŽππ€ π€πˆππ” πŸ’πŸ™ˆπŸ’ž:  76

Akacheka akisema “kwa ulivyonichosha sitaki hata ufanye nini.” Nikasema “ya kweli hayo?” Akacheka akisema “kwanza haramu. “ Tukacheka nikisema “unajua nasubiriwa na leo nawahi kutoka kwaajili ya maandalizi ya kesho.” Akanitazama akasema “hata mimi nawahi kutoka naenda msaidia totoo kujiandaa. Sasa sikia ukitoka fanya unaloweza kanisubiri pale kona ya kanisani. Mimi nakufuata hapo chapu nakupeleka saluni nzuri mama yangu nilikuwa nampeleka hapo. Ukapendeze.” Nikamuuliza “tunaenda wote saluni?” Akaniambia akicheka “haya nenda ubishi ni haramu.” Nikacheka na kuanza kutoka. Wakati natoka tu, nikakutana na mfanyakazi mwingine mlangoni na yeye ndiyo alikuwa anaingia. Natamani ungemuona alivyokuwa ananitazama. Nikasema wewe usinitanie, mimi nikarudi

Soma zaidi

Post a Comment

0 Comments