
alimrudisha nyumbani na yeye akaondoka. "Bibie ndo unarudi saizi, umekosa mambo mazuri, alisema Dora. "Mambo gani hayo?" aliuliza Mia. "Mpenzi wake na Judith alituletea biriani na chips," Dora alimtambia Mia. "Asikudanganye, hakuna mtu yoyote aliyekuja hapa leo," alisema Judith. "Aaah kwanini unaharibu mchezo, nilitaka tu aseme alienda wapi na boss Gael, Dora alikasirika. "Kumbe hiyo ndo michezo yenu! Tulienda tu kituo cha yatima kule Tumaini na baada ya hapo ndo akanirudisha nyumbani." Wote walimcheka Dora. "Mia, leo tunatoka! Tunaenda club usiku," alisema Judith huku anatabasamu. "Sawa, hata mimi nitaenda, nataka kuona hizo starehe za club mnazozisema kila mara, alijibu Mia
0 Comments