
" kama nilivyojitambulisha hapo mwanzo naitwa Angelo na nimekuja hapa kwa agizo la Jerry. " Jerry huyu Double J? " Ndio huyo huyo. Lina alitulia kimnya huku akiwa anajiuliza Jerry amejuaje kama yupo pale kituoni. " Tunaweza kufuatana pamoja. " Kwenda wapi? " Aliniambia tukitoka kituoni tuende pamoja nyumbani kwake. " Sawa lakini nataka kumtafuta shangazi yangu kwanza. " Sawa fanya hivyo. Lina alichukua simu yake na kupiga simu kwa shangazi yake. Simu iliita mara mbili kisha ikapokelewa. " Vipi lina? Shangazi yake aliuliza kwa shauku. " Shangazi nimetoka polisi kwa dhamana , wewe upo wapi? " Nimechukua chumba gesti
0 Comments