
. ILIPOISHIA.... Wakiwa katikati ya mazungumzo yao mazito, mwanamke mmoja mwenye nywele ndefu aliyevaa miwani myeusi, aliketi meza ya jirani. Alikuwa akiwafuatilia kwa makini, huku akijifanya anasoma gazeti. Macho yake yalikuwa makali kama ya mpelelezi. Hakuwa mgeni katika sakata hili la Chacha. Ni yule mwanamke mvamizi. Yuko hapa tena kuendeleza misheni yake. SASA ENDELEA.... Mwanamke huyu aliyekaa pembeni akifuatilia kwa kina maongezi kati Madam Sandra na Dkt Marry anaitwa Rahma. Hilo ndilo jina alilopewa na wazazi wake. Hayuko hapa kwa bahati mbaya bali anapambana kuufichua ukweli wa siri nzito iliyopo nyuma ya Madam sandra na Dkt Marry. Rahma ni nani?
0 Comments