
ILIPOISHIA..... Simu ya Dkt Marry ikaendelea kuita mfululizo, Madam Sandra akapiga na kupiga tena lakini wala haikupokelewa. Mwisho akaandika ujumbe huu wa maandishi. ,,,,,Hupokei simu kuna jambo haliko sawa ni kuhusu lile swala tulilifanya mwaka juzi, nipigie haraka,,,,,, SASA ENDELEA... Baada ya kuumaliza mchezo wa kikubwa jikoni Onesmo alijikongoja kimya kimya akatoka kwenda sebuleni. Akahakikisha anasawazisha sura yake na mavazi yake ili asiwe na chembe ya mashaka mbele ya mjomba wake. Alipofika sebuleni, alikaa juu ya sofa mbali kidogo na mjomba P, akijifanya yuko bize kupekua simu yake. Alijitahidi kuonekana mnyenyekevu, mwenye nidhamu ya heshima kwa Mjomba wake, lakini ndani
0 Comments