
"Hayaa niambie sasa mke wangu ina maana zile sauti ndio ulikuwa unazisikiliza pale mlangoni?" Lukasi aliuliza baada ya kufika chumbani kwao na kumketisha mkewe kitandani. "Nisamehe Mume wangu, wakati nilipokuwa narudi kutoka chooni kukojoa ndio nikasikia sauti zile chumbani kwa Japhet nikaamua kusimama na kusikiliza" Flora alijitetea akijisikia aibu. Lukasi alishusha pumzi ndefu na kujikuna kichwa chake halafu akauliza: "Bila shaka ile sauti ya msichana inayosikika huko chumbani kwa Japhet ni ya Rozi na sio sauti ya msichana mwingine yeyote?" Lukasi alimuuliza mke wake. "Ndio mume wangu ile ni sauti ya Rozi" Flora alijibu. "Ok hakuna shida mke wangu, naomba
0 Comments