
Kweli bwana, jumatatu ya asubuhi Sadru alinifata chumbani kwangu. Mi nilikuwa najiandaa kwenda shule, akanisalimia ila mi bado namuonea aibu mana sijamzoea kabisa. Nae ukaribu wake wa gafla ndo ukazidi kabisa kunitoa kwenye mstari. "Umeamkaje?" "Nashkuru Mungu niko sawa." "Leo nakupeleka mimi shule." Nilishtuka kidogo lakini nilikubali tu kupelekwa na kaka angu maana hata sijui kwanini nilijikuta natamani kuwa nae kweli. Nilijiandaa fasta hiyo siku, sikutaka kumchelewesha maana najua kabisa anasafari. Natoka tu nikamkuta nje ya malango wangu, akanambia, "Umewahi sana sikutegemea." Haa, nikatabasam tu kwa aibu tukawa tunatoka. Sadru akamwambia dereva kuwa hiyo siku atanipeleka mwenyewe. Mama ndo alikuwa
0 Comments