MREMBO KIPOFU 15

MREMBO KIPOFU 15

Nilianza kuomba omba tena kwenye foleni. Ile ndoto ya kufanyiwa upasuaji ilipotea kabisa, akili yangu mpya ilikuwa inaniambia kuwa nikusanye pesa nitafute biashara yangu, siwezi kuishi maisha ya kuomba omba mpaka uzeeni. Nilipingana sana na ile akili iliyokuwa inaniambia mimi nitaishi na kufa kama bibi yangu tu. Hakuna siku niliyopumzika, hakuna siku niliyohema, hakuna siku nilichoka. Sikuwa na W/end, nilihakikisha nina isaka pesa ili tu niweze kuanzisha kibishara changu mimi mwenyewe, mambo ya kuomba sikuwa nayapenda. Ilipita miezi miwili nikiwa nalala nje ya kanisa moja kubwa tu, nilifanya vile ili kupata angalau ulinzi nisije nyanyaswa tena. Nilihesabu pesa zangu nikaona

Soma zaidi

Post a Comment

0 Comments